Huduma Ya Uzazi na Kujifungua

Posted on: April 24th, 2024

Hospitali inatoa huduma za uzazi na kujifungua. Huduma hizi hutolewa kila siku na madaktari bingwa wa magonjwa ya uzazi na akina mama. Wananchi wanashauliwa kufuata utaratibu wa rufaa kabla ya kuja kutibiwa Hospitali Ya Mkoa. Pia tunapenda kuihimiza jamii hasa wakinamama wajawazito kuhudhuria kliniki katika vituo vya afya vilivyo jirani nao. Mama mjamzito unasisitizwa kujifungulia hospitali.